Kampuni, mashirika na taasisi
mbalimbali zimeshauriwa kuhifadhi kumbukumbu zao katika kituo cha taifa
cha kuhifadhia kumbukumbu DATA CENTRE ambacho kinatarajiwa kuanza rasmi
kuhifadhi kumbukumbu mwezi Mei mwaka huu.
Rai
hiyo imetolewa na waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi Profesa
Makame Mbarawa wakati alipotembelea kituo hicho cha Taifa cha kuhifadhia
kumbukumbu kilichopo Kijitonyama jijini Dar es Salaam ambapo amesema
itashangaza sana kwa mtanzania kwenda kuhifadhi kumbukumbu nje ya nchi
wakati tayari taifa limeshaanzisha kituo cha kisasa kwa madhumini hayo
Profesa Mbarawa amesema katika biashara
ya vituo vya kuhifadhi kumbukumbu, kituo hicho ni kikubwa kuliko vyote
Afrika Mashariki na Kati.
Aidha Profesa Mbarawa amaesema serikali
ina mpango wa kujenga vituo vingine viwili vya kuhifadhia kumbumbu
katika mkoa wa Dodoma na Zanzibar huku akiwahakikishia wananchi na wadau
mbalimbali kuwa kumbumbuka hizo zitahifadhiwa katika hali ya usalama
bila usumbufu wowote.
News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook, Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.
RELATED POSTS
MAKAMPUNI YASHAURIWA KUTUMIA ‘DATA CENTRE’
Reviewed by Newspointtz
on
06:52:00
Rating: 5
0 comments:
Post a Comment