Wizara ya Nishati na Madini Inaendesha
mkutano na wafanyabiashara wa mafuta nchini ambao utalenga kuibua fursa
zitakazo jitokeza katika mradi wa ujenzi wa bomba la Mafuta litakalo
jengwa kuanzia HOIMA
nchini Uganda hadi bandari ya Jijini Tanga.
Akizungumza na wanahabari Katibu mkuu wa
Wizara ya Nishati na Madini Profesa Justin Ntalikwa amebainisha fursa
zitakazojitokeza kupitia mradi huo kuwa ni pamoja na kupata tenda, ajira
kwa vijana, kodi
itakusanywa kupitia mradi huo wa ujenzi.
“Mradi huo utapitia nchini lakini pia
utaibua fursa mbalimbali zikiwemo ajira,tenda na utaongeza pato la Taifa
kupitia ukusanyaji wa kodi”. Alisema
Katibu
Aidha Ntalikwa ameongeza kuwa ujenzi huo
utaendeshwa kwa miezi thelathini na sita (36) na utaanza mara tu baada
ya makubaliano baina ya Tanzania, Kenya na Uganda ambapo dalili
zinaonesha wazi kuwa bomba litajengwa Tanzania kulingana na sifa ya nchi
hiyo kuwa na Vigezo husika kama Uzoefu,Amani na Ulinzi.
News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook, Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.
RELATED POSTS
TAARIFA MPYA KUHUSU UJENZI WA BOMBA LA GESI UGANDA-TANZANIA
Reviewed by Newspointtz
on
18:05:00
Rating: 5
0 comments:
Post a Comment