WATOTO wenye ulemavu mbalimbali 409
wanaolelewa katika kituo jumuishi kilichopo Buhangija Manispaa ya
Shinyanga wamedaiwa kukosa upendo dhidi ya wazazi na walezi
kwenye familia zao baada ya kuwatelekeza kwa muda mrefu.
Kwani wazazi
wamekuwa hawatoi ushirikiano dhidi yao hata katika kipindi hiki cha sikukuu ya
pasaka wameshindwa kujitokeza nakuwafarij huku wakikubwa na changamoto ya uhaba
wa mavazi na mlo kamili.
Hayo
yalisemwa jana na mwalimu Sasu Nyanga
msaidizi msimamizi wa kituo hicho baada ya familia ya muuguzi mstaafu Anna Mwalongo na mumewe Josephat Mwalongo
kutoa msaada wa nguo,kilo 100 za mchele
na mbuzi mmoja katika kituo hicho.
Nyanga
alisema kuwa kituo hicho kwa sasa kina jumla ya watoto 409 aliwataka wazazi na walezi wajenge upendo
kwa watoto hao kwani wameonekana kukosa upendo
kwasababu ya kushindwa kutoa ushirikiano tangu wanapowaleta na kwenda moja kwa moja bila kurudi
nakuwajulia hali zao.
“Kituo hiki
kinawatoto wakuanzia miaka miwili
hadi 12
wakiwa 70 wamekosa upendo wa
dhati kwa wazazi wao kwani tangu
wamewaleta kituoni hapa wameshindwa kurudi
kuwajulia hali nakuwafariji hasa
Kipindi hiki cha sikukuu ya pasaka pia
wana changamoto ya kukosa mavazi,chakula
na malazi”alisema mwalimu Nyanga.
Anna
Mwalongo ambaye ni muuguzi mstaafu na
msemaji kwa niaba ya familia yake alisema kuwa wameguswa kutoa msaada wa vitu
hivyo kutokana na watoto hao wenye haki ya kupata stahiki zote kama binadamu
wengine wapate hasa kipindi hiki cha
sikukuu ya pasaka.
Hata hivyo
waliendelea kutoa msaada wa nguo katika
kambi ya kulelea wazee wenye maradhi ya ukoma wapatao 23 ambao wanachangamoto ya mavazi pia aliwaomba wadau wengine wasiishie msaada wa vyakula bali waangalie na changamoto
zingine zinazowakabili wazee hao ni nyingi.
Baadhi ya wazee hao Hellen Masanja na Shija Nipuge walishukuru msaada huo huku wakieleza changamoto ya ukosefu wa nishati ya umeme,nyumba kuwa na nyufa na kuvuja kipindi cha mvua ikiwemo kukosa matibabu
0 comments:
Post a Comment