Mume
na mke wakulima na wakazi wa kijiji cha Tambukareli, Tarafa ya Itigi,
wilaya ya Manyoni mkoani Singida, wameuawa kikatili kwa kukatwa katwa
kwa mapanga sehemu mbali mbali za miili yao na watu wasiofahamika.
Wanandoa
hao ni Mbulalina Shomi (80) na mke wake Joyce Mathayo (70), ambapo
inadaiwa kuwa wameuawa na mtoto wa kambo Henry Yoweli Malugu (55) ambaye
ni mtoto wa marehemu Joyce Mathayo.
Kamanda
wa jeshi la polisi mkoa wa Singida, ACP Thobias Sedoyeka, alisema tukio
hilo la kusikitisha, limetokea Aprili, 10 mwaka huu saa sita za usiku
huko katika kijiji cha Tambukareli.
Alisema
siku ya tukio wakati wanandoa hao wamelala, walivamiwa na watu
wasiofahamika baada ya kuvunja mlango wa mbele wa nyumba yao na kuingia
ndani na kutekeleza azma yao.
Sedoyeka
alisema uchuguzi wa awali umebaini kuwa muuaji huyo wanawania mifugo
mingi ambayo idadi yake haijafahamika,iliyokuwa inamilikiwa na marehemu
Mbulalina.
Alisema wanamshikilia Henry na baada ya kumaliza upelelezi, atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma inayomkabili.
Katika
tukio la pili,Kamanda huyo alisema wanawashikilia Wende Makoye (28) na
Gidangida Ganagu (30) wakazi wa kitongoji cha Midimbwi kijiji cha
Munguli, Tarafa ya Kirumi, Wilaya ya Mkalama mkoa wa Singida,kwa tuhuma
ya kumiliki lita 20 za pombe haramu ya Moshi/Gongo.
Alisema watuhumiwa hao walikamatwa wakati wa msako wa kukamata watu wanaojihusisha na vitendo vya uhalifu.
Wakati
huo huo, Sedoyeka alisema kuwa jumla ya bunduki aina ya Rifle 30,
Bastola 35 na shotgun,zimeisha hakikiwa kati ya aprili mosi na sasa.
“Changamoto
inayoendelea kujitokeza katika zoezi hili la kuhakiki silaha,ni
muitikio mdogo wa wananchi kutokana na upatikanaji wa taarifa
inayosababishwa na hali ya kijiografia ya mkoa wetu,” alisema.
0 comments:
Post a Comment