Mkuu
wa mkoa wa Singida, Mhandisi Mathew Mtigumwe amefanya ziara ya
kushutukiza katika soko la wakulia na wafanyabiashara wa vitunguu wa
soko la kimataifa Misuna ambapo alimpa siku 14 Kaimu Mkurugenzi wa
manispaa ya Singida, Deus Lisige awe amejenga kibanda kwa ajili ya wauza
vitunguu hao, waweze kujihifadhi wakati wa mvua na jua.
Mkuu
wa mkoa wa Singida, Mhandisi Mathew Mtigumwe (kulia mwenye miwani)
akimwagiza Kaimu Mkurugenzi wa manispaa ya Singida, Deus Lisige
(anayeaangalia kamera), kwamba ahakikishe ndani ya siku 14 awe amejenga
kibanda kwa ajili ya wakulima na wafanyabishara wa vitunguu soko la
kimataifa Misuna, waweze kujihifadhi wakati wa mvua na jua.
Mwenyekiti
wa SACCOS ya wafanyabiashara wa vitunguu soko la kimataifa la Misuna
mjini Singida, Joseph Nandoo (mwenye fulana ya misitari), akimweleza
jambo Mkuu wa mkoa wa Singida, mhandisi Mathew Mtigumwe (mwenye suti
nyeusi), aliyetembelea soko hilo.
Mkuu
wa mkoa wa Singida,mhandisi Mathew Mtigumwe, akikagua soko la vitunguu
la kimataifa la Misuna mjini Singida alipofanya ziara ya ghafla ya
kikazi na kuagiza manispaa kujenga soko la kisasa la vitunguu,ili
kuvutia wakulima ndani na nje ya mkoa,kuuzia vitunguu vyao.
Baadhi
ya wakulima, wafanyabiashara na vibarua katika soko la vitunguu la
kimataifa la Misuna, wakiendelea na majukumu yao wakati mkuu wa mkoa wa
Singida,mhandisi Mathew Mtigumwe alipolitembelea soko hilo.(Picha zote
na Nathaniel Limu)
0 comments:
Post a Comment