Wizara
ya Afya, Ustawi wa Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kupitia Waziri wake,
Mhe. Ummy Mwalimu imeeleza kuwa inajipanga kufanya utafiti ili kuona ni
jinsi gani wataweza kumaliza ugonjwa wa Kipindupindu.
Akizungumza
na waandishi wa habari, Mhe. Ummy Mwalimu amesema haikuwahi kutokea
awali kwa Kipindupindu kuwepo nchini kwa kipindi kirefu kama ilivyo sasa
na hivyo wameona ni vyema kufanya utafiti kuona kwanini ugonjwa huo
bado unaendelea kuwepo nchini.
Amesema
utafiti huo utafanyika kwa kipindi cha wiki sita na baada ya hapo
watazishirikisha ofisi zilizo juu ya wizara hiyo ili kuona ni jinsi gani
wataweza kusaidiana kumaliza Kipindupindu.
Waziri Ummy Mwalimu akizungumza na waandishi wa habari kuhusu ugonjwa wa Kipindupindu.
“Haikuwahi
kutokea kipindupindu kuwepo nchini kama ilivyo sasa kilikuwa kikikaa
sana nchini ni miezi miezi miwili au mitatu lakini hiki cha sasa hivi
kinakaribisa miezi saba sasa kwahiyo tumeona kwanza tufanye utafiti,
“Baada
ya utafiti tutashirikisha ofisi ya waziri mkuu na ofisi ya rais na hapo
tutaona ni hatua gani itachukuliwa kwa pamoja tukishirikiana,” amesema
Mhe. Mwalimu katika mkutano huo.
Aidha
ameeleza kuwa wagonjwa wapya wa Kipindupindu kwa kuanzia Aprili, 4 hadi
10 wamepungua kutoka 531 kwa wili iliyotangulia hadi kufikia 368, na
mkoa wa Mara ukiongoza kwa kuwa na wagonjwa 128 na kifo kimoja huku
mikoa ya Njombe na Ruvuma ikiendelea kuwa salama kwa kutokuripoti
mgonjwa yoyote.
Baadhi
ya watumishi wa Wizara ya Afya, Ustawi wa Jamii, Jinsia, Wazee na
Watoto waliohudhuria mkutano wa Waziri wa Afya, Mhe. Ummy Mwalimu na
waandishi wa habari.
Waziri Ummy akizungumza na waandishi wa habari.
0 comments:
Post a Comment