NEWSPOINTTZ.BLOGSPOT.COM

Snura aomba radhi kwa wimbo uliofungiwa Tanzania


 Msanii Snura Mushi ambaye wimbo wake wa Chura ulipigwa marufuku


 Snura amewaonesha kile alichosema ni cheti.

Msanii Snura Mushi ambaye wimbo wake wa Chura ulipigwa marufuku na serikali ya Tanzania jana ameomba radhi na kuahidi kutekeleza maagizo ya serikali.

Wimbo huo ulipigwa marufuku na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ambayo ilisema "maudhui ya utengenezwaji wa video ya wimbo huo “haiendani na maadili ya Mtanzania.”
Mamlaka hiyo ilisema kazi hiyo inadhalilisha tasnia ya muziki.
Serikali ilipiga marufuku maonyesho yote ya hadhara ya Snura hadi pale atakapokamilisha usajili wa kazi zake za Sanaa katika Baraza la Sanaa la Taifa (Basata).

Akizungumza na wanahabari akiwa ameandamana na meneja wake, Snura amesema amechukua hatua na kusajiliwa rasmi kwa ajili ya shughuli za kisanii.
Share on Google Plus

News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook , Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.

0 comments:

Post a Comment