
Yusuph Manji amechaguliwa kwa awamu nyingine kuwa mwenyekiti wa Timu ya Young Africans ‘Yanga’ pamoja na makamu wake Clement Sanga.
Matokeo rasmi ya uchaguzi mkuu wa 2016 uliofanyika jana June 11 2016 katika ukumbi wa Diamond Jubilee Dar es Salaam yametangazwa leo June 12 2016, ambapo Yusuph Manji na Clement Sanga ameibuka kidedea ambapo Manji kashinda kwa jumla ya kuraza ndio 1468, hapana 0 na kura zilizoharibika zilikuwa 2.

kwa upande wa makamu wake Sanga ameshinda kwa jumla ya kura 1428 kati ya kura 1508 zilizopigwa huku mpinzani wake Titus Ossoro akipata kura 80 pekee
0 comments:
Post a Comment