NEWSPOINTTZ.BLOGSPOT.COM

JPM-WATU WALIZOEA ‘MADILI ‘ SANA

 rais magufuli

RAIS John Magufuli amesema watu wanaolalamika kwamba fedha hazionekani mitaani ni watu waliozoea ‘kupiga dili’ (kujipatia fedha isivyo halali).

Ameeleza kuwa wapo wananchi walioficha fedha ili wasibainike kuwa na kiwango kikubwa na kuwataka wazitoe, vinginevyo anaweza kuchapisha noti mpya na hizo zilizofichwa zikaoza.

Akifungua Mkutano wa 14 wa Siku ya Wahandisi nchini uliofanyika Dar es Salaam jana, Dk Magufuli alioneshwa kukerwa na tabia ya watu waliozoea, kuifanya nchi kama shamba la bibi kwa kutapanya mali za umma huku baadhi ya watendaji wakikiuka maadili ya uongozi kwa maslahi binafsi.

“Tanzania imechoka kuibiwa na kuchezewa kwa sababu kila mahali ni dili, ukigeuka huko wanapiga dili, huku ni dili, serikali kupitia mashirika ya umma mbalimbali ilikuwa haipati hela kwa sababu ya dili, ni dili tu kila mahali, sasa kwa mwendo huu wa kwangu hizo dili basi,” alisisitiza Rais Magufuli.

Akizungumzia wananchi walioficha fedha, Rais Magufuli aliwataka wazitoe fedha hizo na ziende kwenye mzunguko wa fedha na kwenye miradi ya maendeleo, na kusisitiza kuwa anaweza kuamua kubadilisha noti na hizo zilizofichwa zikawaozea kwenye magodoro.

Share on Google Plus

News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook , Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.

0 comments:

Post a Comment