NEWSPOINTTZ.BLOGSPOT.COM

MWAKYEMBE- KATIBA MPYA INAKUJA

 Image result for picha ya mwakyembe

SERIKALI imesema itafanya mapinduzi makubwa katika sekta ya sheria, yatakayowezesha kufikiwa kwa mchakato wa Katiba Mpya, kukomesha rushwa, kuipa meno Sheria ya Ndoa na Mirathi na kuipa majukumu Mahakama ya Rushwa na Mafisadi.

Maeneo mengine yatakayofanyiwa kazi ili kuboreshwa ni Sheria ya Mitandao, Sheria ya Kupata Taarifa, lakini pia kupelekwa bungeni kwa Muswada wa Sheria ili kuwasaidia wananchi wasio na uwezo wa kupata huduma za kisheria.KATIBA YA JAMURI YA MUNGANO WA TANZANIAHayo yalisemwa juzi usiku na Waziri wa Sheria na Katiba, Dk Harrison Mwakyembe wakati akizungumza katika kipindi cha ‘Tunatekeleza’ kinachorushwa hewani na Kituo cha Televisheni cha TBC1, kwa lengo la kuainisha shughuli mbalimbali zinazofanywa na serikali katika kuharakisha maendeleo ya wananchi.

Katiba Mpya Inayopendekezwa

Akizungumzia Katiba Mpya Inayopendekezwa, Mwakyembea alisema mchakato wa kupata Katiba mpya ya Tanzania, ambao uliachwa kiporo na Serikali ya Awamu ya Nne, upo pale pale ingawa utekelezaji wake utakwenda polepole.

Alisema uthibitisho kuwa mchakato huo, utaendelezwa na Serikali ya Awamu ya Tano ni kauli iliyotolewa na Rais John Magufuli mara kadhaa kwamba serikali yake itaendelea na mchakato huo ili kupata Katiba mpya.

“Na mimi (Mwakyembe) niseme vivyo hivyo, nina uhakika kuwa litafanyika hivyo, alichokifanya Rais ni kuzipa nguvu mamlaka husika ili kuendelea na mchakato huo bila kuingiliwa,” alisema Dk Mwakyembe.

Share on Google Plus

News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook , Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.

0 comments:

Post a Comment