Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Dkt. John Pombe Magufuli jana aliungana na waumini wa Parokia ya Toleo
la Bwana iliyopo katika Jimbo Katoliki la Arusha kusali ibada ya
Jumapili, ambapo katika salamu zake amewaomba watanzania kuendelea
kuiombea nchi yao ili kazi anayoifanya ya kukabiliana na matatizo
yanayowakabili watanzania wanyonge ifanyike kwa mafanikio.
Dkt. Magufuli amesema hayo
alipokaribishwa na Mwenyekiti wa Parokia hiyo Bw. Philemon Mushi
kuwasalimu waumini wa kanisa hilo, mara baada ya kumalizika kwa ibada ya
Jumapili ya kupaa kwa Bwana.
“Niko pamoja na nyinyi ndugu zangu
watanzania na wana Arusha wote, napenda kuwaahidi tena sitawaangusha,
nitasimama mbele kuwatetea masikini, siku zote nitakuwa upande wenu,
siku zote nitatembea na nyinyi, nasema kwa dhati kabisa na nataka
muamini hilo kwamba sitawaangusha” amesema Rais Magufuli huku
akishangiliwa na waumini walioshiriki ibada hiyo.
Rais Magufuli amewahakikishia
watanzania wote kuwa atahakikisha ahadi zote alizoziahidi anazitekeleza
na amewaomba watanzania wote kuungana na kushikamana ili kufanikisha
juhudi za kuijenga Tanzania bora.
News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook, Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.
RELATED POSTS
JPM:Kutumbua majibu sio ukatili
Reviewed by Newspointtz
on
09:13:00
Rating: 5
0 comments:
Post a Comment