NEWSPOINTTZ.BLOGSPOT.COM

Halima Mdee amtaja rapper wa Bongo anayemkubali zaidi

Mdee-Halima

Kama umejibu Roma Mkatoliki basi ubashiri wako upo sahihi.
“Nampenda Roma Mkatoliki kwasababu anaimba hali halisi, unajua wasanii ni vioo vya jamii sasa inategemea msanii anataka atumike vipi, atumike kibiashara peke yake ama atumike katika kuelimisha jamii mambo yanayoendelea katika nchi yake,” Mdee aliamuambia mtangazaji wa kipindi cha Hot Stage cha Jembe FM, Jay Jay.

“Kwahiyo Roma above all, yaani wasanii wote, si Diamond, si Alikiba wote wanaimba mapenzi, ni wasanii maarufu wanapendwa lakini mwisho wa siku wanaimba mapenzi na mapenzi hayasaidii nchi, kinachosaidia nchi ni wewe kuangalia namna gani unaweza kutumia taalum yako kama kioo cha jamii.

Watu wanakusikiliza ili kuweza kupeleka meseji, sio kupeleka meseji ya uchochezi bali ya uelewa, kucreate awareness kwa wananchi ambao wanawasikiliza wasanii kwa kiasi kikubwa. Kwahiyo kwangu Roma Mkatoliki amekuwa akifanya kazi nzuri kutumia sanaa kama kuburudisha lakini at the same time kuelimisha.”
Share on Google Plus

News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook , Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.

0 comments:

Post a Comment