NEWSPOINTTZ.BLOGSPOT.COM

RONALDO AIFIKIA REKODI YA MFUNGAJI WA MUDA WOTE MICHUANO YA EURO


Ronaldo-Platini 2
Cristiano Ronaldo inawezekana hafanyi vizuri kwenye michuano ya Euro 2016, lakini licha ya kutocheza katika kiwango chake kinachotarajiwa, bado anauwezo wa kutengeneza na kuvunja rekodi.
Kuvunja rekodi imekuwa ni sehemu ya maisha ya ronado, mara kadhaa amefanya hivyo kwenye klabu yake ya Real Madrid, baada ya goli lake la kichwa dhidi ya Wales amefanikiwa pia kufikia rekodi iliyowekwa na Michel Platini miaka kibao iliyopita.
Ronaldo aliruka juu mithili ya mcheza kikapu Lebron James na kukutana na krosi ya Gueirrero kisha kuuzamisha mpira kambani.
Ronaldo-Platini
Goli hilo liliipa Ureno uongozi wa goli 1-0 dhidi ya Wales kwenye mchezo wa nusu fainali ya Euro 2016 na kumfanya Ronaldo awe sambamba na rekodi ya legend wa Ufaransa Michel Platini ya kufunga magoli magoli 9 kwenye michuano ya Mataifa ya Ulaya.
Ronaldo alifunga goli lake la kwanza kwenye michuano ya Euro mwaka 2004.
Anahitaji goli moja ili kuwa mfungaji wa muda wote kwenye michuano ya Euro.
Share on Google Plus

News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook , Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.

0 comments:

Post a Comment