NEWSPOINTTZ.BLOGSPOT.COM

MV Magogoni kuanza kazi rasmi mwezi huu

 

magogoni

SERIKALI imesema ukarabati wa kivuko cha Mv Magogoni jijini Dar es Salaam, upo katika hatua za mwisho na ifikapo katikati ya mwezi huu kitaanza tena kutoa huduma.

Kivuko hicho kina uwezo wa kubeba abiria 2000 na magari 60 na kinatoa huduma eneo la Feri na Kigamboni. 

 Katibu Mkuu, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (anayesimamia ujenzi), Joseph Nyamhanga, aliyasema hayo jana alipotembelea eneo la Mamlaka ya Bandari (TPA) linalojulikana kama ‘Dock Yard’ kuangalia maendeleo ya uundwaji na ukarabati wa vivuko vitatu vya Mv Magogoni (cha zamani) na vivuko vipya vya Mv Magogoni na Mv Tanga.

Nyamhanga alisema ukarabati wa kivuko cha Mv Magogoni (cha zamani), unaendelea vizuri na upo katika hatua za kukamilika hivyo wananchi wataondokana na usumbufu wa usafiri katikati ya mwezi huu.

Aidha, alisema uundwaji wa kivuko kipya cha Mv Magogoni chenye uwezo wa kubeba tani 150, abiria 800 na magari 22, unaendelea vizuri na mpaka sasa umekamilika kwa asilimia 50 hivyo Oktoba mwaka huu kitakuwa kimekamilika na kuanza kutoa huduma.

Share on Google Plus

News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook , Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.

0 comments:

Post a Comment