NEWSPOINTTZ.BLOGSPOT.COM

RONALDO ANAVUNJA REKODI ALIZOWEKA MWENYEWE

Ukijaaliwa kipaji, kinachofuata ni juhudi zako binafsi kuhakikisha unafikia malengo pia ukifikia malengo ya awali lazima ujiwekee malengo mapya. Kama ilivyokuwa kwa Cristiano Ronaldo, baada ya kutimiza malengo ndani ya Manchester United akaamua kutimkia Real Madrid ambako ametimiza malengo hadi yale ambayo hakuwa amejipangia.

AMEFANYA NINI TENA CR7?

Mfungaji bora wa muda wote Real Madrid  Cristiano Ronaldo amevunja rekodi nyingine akiwa santiago Bernabeu. Magoli aliyofunga jana dhidi ya Valencia yamefikia 200 akicheza katika dimba la SANTIAGO BERNABEU baada ya kucheza michezo 171 kwa misimu saba akiwa Hispania, Magoli 149 ameyafunga akiwa katika michuano ya ligi kuu Hispania wakati 40 akiyapata michuanao ya UEFA, mengine 10 yakipatikana kwenye kombe la mfalme yaani Copa de rey huku goli 1 likiwa Super cup.

Ronaldo ameanza safari yake ya kufunga katika uwanja huo akiifunga Deportivo. Lakini pia amefunga mabao mengi kwenye mchezo dhidi ya Granada alipopiga goli 5 peke yake msimu wa 2014/15. Mahesabu yanaonesha kasi ya Ronaldo ya kufunga ni goli 1.6 kwa kila mchezo.

Hapa Tanzania rekodi ya Mohamedi Hussein “Mmachinga” ya magoli 26 kwa msimu mmoja inabaki kuwa ngumu kuivunja wakati Ulaya kila mechi watu wanategemea kuvunja rekodi .

Share on Google Plus

News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook , Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.

0 comments:

Post a Comment