NEWSPOINTTZ.BLOGSPOT.COM

Kigogo wa Madawa ya Kulevya Atiwa Mbaroni


Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam inawashikilia watu wawili kwa tuhuma za kukutwa na dawa za kulevya aina ya heroine zenye uzito wa kilo moja, akiwamo anayedaiwa kuwa kigogo wa biashara ya dawa hizo nchini.

Kamanda wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Simon Sirro aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa, juzi saa 1.15 usiku katika maeneo ya Mbezi Beach, walimkamata mtuhumiwa wa kwanza akiwa na gari baada ya kumpekua alikutwa na dawa hizo za kulevya. 

Alisema walipomhoji zaidi, alidai kuwa dawa hizo siyo zake, bali za tajiri yake anayeishi Mikocheni jijini hapa ambaye wali panga kukutana naye maeneo ya Mbezi Beach kwa ajili ya kukabidhiana.

Alisema upelelezi unaendelea na utakapokamilika, watuhumiwa watafikishwa mahakamani. 

Kukamatwa kwa kigogo huyo na msaidizi wake ni mafanikio ya jeshi hilo ambalo hivi karibuni lilimkamata kigogo mwingine muuza ‘unga’ jijini hapa hivi karibuni. 

Wakati huohuo,Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam kupitia kitengo chake cha usalama Barabarani limekamata magari mbalimbali kwa makosa ya usalama barabarani 

Jumla ya Tshs. 577,831,000 zimekusanywa ikiwa ni tozo kwa makosa hayo kwa mida wa siku 12, kuanzia 07/03/2016 hadi tarehe 18/03.2016.

Kamanda Sirro amewataka madereva kuwa makini na waangalifu pindi wawapo barabarani ili kuepuka adhabu zitolewazo ili vipato hivyo viwasaidie katika maisha yao ya kila siku. 

chanzo>mpekuzi
Share on Google Plus

News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook , Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.

0 comments:

Post a Comment