Rapper
wa muziki nchini Tanzania, Baghdad, ameamua kuandaa mixtape aliyo iita
Old is Gold ambayo imekusanya nyimbo za zamani nakuzirudia tena studio
ikiwemo Mtazamo ya Solo, Nikusaidiajeya Profesa Jay na nyinginezo ambazo kwa mujibu wake Baghdad amesema tayari ameshapewa ruhusa ya kuendelea kuzifanya.
Lakini inasemekana kuna maneno ambayo
Baghdad ameyazungumza yakasababisha mfarakano kati yake na Babu Tale
kitu ambacho kime mpelekea Babu Tale amtoe kwenye kundi la Whatsapp
kundi ambalo limekusanya baadhi ya wasanii wa Tanzania.
Kwenye remix ya Mtazamo aliyoimba
Baghdad kunamistari ambayo ameimba “Game ishakuwa yawadau, Tale anaweza
kukufanya media house ikuzarau, Kama hauna hela kajiunge Mkubwa Fela.”
Akizungumza na mtembezi.com kuhusu suala
hilo meneja huyo wa Tip Top Connection na Diamond Plutnumz Hamisi Tale,
Babu Tale amesema kuwa hayupo tayari kumzungumzia rappa Bagh Dad.
News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook, Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.
RELATED POSTS
Siwezi kumzungumzia Baghdad-Babu Tale
Reviewed by Newspointtz
on
06:44:00
Rating: 5
0 comments:
Post a Comment