NEWSPOINTTZ.BLOGSPOT.COM

VIGOGO 150 WATEKELEZA AGIZO LA MAKONDA

 

WAKATI zaidi ya watu 150 wakijitokeza kuhakiki silaha zao, kutii agizo la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai, Kamishna wa Polisi, Diwani Athumani amesema uhakiki huo sasa unafanyika nchi nzima.

Kamishna Athumani amesema hayo jana alipozungumza na waandishi wa habari, huku akikataa kutaja majina ya vigogo waliojitokeza kuhakiki silaha zao kwa sababu za kiusalama.

“Baada ya Mheshimiwa Rais John Pombe Magufuli kufanya uhakiki wa silaha zake hivi karibuni, watu zaidi ya 150 wakiwemo viongozi mbalimbali wa Serikali, viongozi wastaafu, mabalozi na wabunge wa nchi mbalimbali wamejitokeza,” alisema.

Mbali na vigogo hao, Kamishna Athumani amesema wananchi wengine wameonesha nia ya kufanya hivyo na kusisitiza kuwa, lengo la uhakiki wa silaha hizo ni kuboresha hali ya usalama kwa kuwajua watumiaji .

Alifafanua kuwa utambuzi huo unafanyika kwa kuwa kunaweza kutokea sababu mbalimbali zitakazofanya wamiliki wa awali wasiendelee kumiliki silaha hizo, ikiwemo vifo na ulemavu.

Share on Google Plus

News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook , Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.

0 comments:

Post a Comment