WAKATI zaidi ya watu 150 wakijitokeza
kuhakiki silaha zao, kutii agizo la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul
Makonda, Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai, Kamishna wa Polisi,
Diwani Athumani amesema uhakiki huo sasa unafanyika nchi nzima.
Kamishna Athumani amesema hayo jana
alipozungumza na waandishi wa habari, huku akikataa kutaja majina ya
vigogo waliojitokeza kuhakiki silaha zao kwa sababu za kiusalama.
“Baada
ya Mheshimiwa Rais John Pombe Magufuli kufanya uhakiki wa silaha zake
hivi karibuni, watu zaidi ya 150 wakiwemo viongozi mbalimbali wa
Serikali, viongozi wastaafu, mabalozi na wabunge wa nchi mbalimbali
wamejitokeza,” alisema.
Mbali na vigogo hao, Kamishna Athumani
amesema wananchi wengine wameonesha nia ya kufanya hivyo na kusisitiza
kuwa, lengo la uhakiki wa silaha hizo ni kuboresha hali ya usalama kwa
kuwajua watumiaji .
Alifafanua kuwa utambuzi huo unafanyika
kwa kuwa kunaweza kutokea sababu mbalimbali zitakazofanya wamiliki wa
awali wasiendelee kumiliki silaha hizo, ikiwemo vifo na ulemavu.
News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook, Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.
RELATED POSTS
VIGOGO 150 WATEKELEZA AGIZO LA MAKONDA
Reviewed by Newspointtz
on
06:48:00
Rating: 5
0 comments:
Post a Comment