NEWSPOINTTZ.BLOGSPOT.COM

Wananchi Singida wahimizwa kufuga kuku wa biashara


Mkuu wa wilaya ya Singida, Saidi Amanzi amewahimiza wakazi wilayani humo kufuga kuku wa kienyeji kibiashara ili waweze kupata kipato kitakachowatoa kwenye lindi la umaskini.
Mkuu huyo wa wilaya, ametoa wito huo juzi wakati akizungumza kwenye zoezi la kugawa msaada wa fedha za mpango wa TASAF 111 kwa ajili ya kunusuru kaya maskini kata ya Ilongero, ambapo zaidi ya shilingi Milioni 13.4 zilitolewa.
Amanzi alisema sio jambo la ufahari mtu mwenye afya njema na ambaye hana ulemavu wa aina yoyote kuendelea kuitwa maskini.
“Niwasihi sana ndugu zangu kataeni kuitwa maskini.Nawahakikishia mtaondokana na sifa hiyo mbaya iwapo tu,mtalichukia jina hilo na kujikita kwenye shughuli halali za kuwaongezea kipato, ikwemo ufugaji wa kuku wa kienyeji na wale wa kisasa,” alifafanua.
Aidha, Amanzi amezitaka kaya zinazopata msaada wa fedha za kugharamia masomo ya watoto wao zihakikishe watoto wao wanasoma kwa bidii ili siku za usoni waweze kuzikomboa kaya hizo kiuchumi.
“Kwa upande wenu ninyi mnaoratibu mpango huu wa TASAF,hakikisheni walengwa kwa maana watu wasiokuwa na uwezo ndio wanaonufaika na sio vingenevyo,” alisema.
Awali mratibu wa TASAF mkoani hapa, Patrick Kasango alisema hadi sasa TASAF 111 imetoa msaada wa jumla ya shilingi Bilioni 14.1 kunusuru kaya maskini 41,321 katika vijiji 280 vya halmashauri sita.
Kasango alisema baadhi ya kaya hizo, zimetumia misaada hiyo kwa ajili ya kuanzisha shughuli za kiuchumi ikiwemo ufugaji wa kuku,bata na mbuzi.
Na Nathaniel Limu, Singida
IMG_4221
Mratibu TASAF mkoa wa Singida Patrick Kasango,akizungumza kwenye hafla ya kugawa fedha za mpango wa TASAF 111 kunusuru kaya maskini katika tarafa ya Ilongero juzi. Wa kwanza kushoto (walioketi) mkuu wa wilaya ya Singida Saidi Amanzi na katikati ni mwenyekiti wa kijiji cha Ilongero.
IMG_4230
Mkuu wa wilaya ya Singida,Saidi Amanzi,akizungumza kwenye hafla ya kugawa fedha za mpango wa TASAF 111 katika tarafa ya Ilongero juzi.Amanzi amewataka wakazi wa wilaya hiyo,kuanzisha ufugaji wa kibiashara wa kuku wa kienyeji,ili waweze kujipatia kipato na hivyo kuondokana na umaskini.Wa kwanza kulia (walioketi) ni mratibu wa TASAF mkoa wa Singida, Patrick Kasango na katikati ni mwenyekiti wa kijiji cha Ilongero.
IMG_4231
Mkuu wa wilaya ya Singida,Saidi Amanzi,akigawa fedha za TASAF mpango wa 111 kunusuru kaya maskini katika kata ya Ilongero.
IMG_4233
IMG_4241
Mkuu wa wilaya ya Singida,Saidi Amanzi (aliyenyoosha mikono), akisisitiza jambo kuhusiana na ujenzi wa zahanati ya kijiji cha Mwahango kata ya Ilongero inayojengwa na TASAF 111. (Picha na Nathanile Limu)
Share on Google Plus

News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook , Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.

0 comments:

Post a Comment