Na.Timotheo Lupembe-Morogoro
Mwenyekiti wa Jumuia ya
Wazazi Taifa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) mh Abdala Bulembo, amekemea tabia ya
Wazazi na walezi wa watoto Nchini kubaka na kuwalaiti watoto wa kufikia hali
inayovunja maadili ya kitanzania.
Hayo yamesemwa jana na Mwenyekiti
wa Jumuia ya Wazazi Taifa ya Chama cha Mapinduzi (CCM) mh Abdala Bulembo katika
maadhimisho ya miaka 61 ya jumuia hiyo kitaifa yaliyofanyika katika Uwanja wa
Jamuhuri Morogoro
“Nikiwa kama mzazi nachukiza
na hii tabia ambayo inashamiri katika sehemu mbalimbali za nchi kiasi ambacho
inavunja mila na tamaduni za watanzania na kuomba ichukuliwe hatua ili
kukomesha tabia hii kwa baadhi ya wazazi” alisema Bulembo
Aidha Mh Bulembo alitumia
siku ya maadhimish ya siku ya Wazazi kuunga mkono jitihada na hatua mbalimbali
ambazo zinaendelea kuchukuliwa na Serikali ya awanu ya tano ya Mh Dr John Pombe
Magufuli.
“Natumia fursa hii kwa niaba
ya Wazazi wote kumpongeza mhesimiwa Rais Dr Magufuli katika jitihada zake za
kuhakikisha miiko na taratibu za kazi zinafuatwa na kufanya nchi yetu iweze kusonga
mbele”aliongeza Bulembo
Siku ya Jumuia ya Wazazi ya
Chama cha Mapinduzi CCM inaazimishwa kila ifikapo tarehe 9 mwezi wa 4 kila
mwaka
0 comments:
Post a Comment