NEWSPOINTTZ.BLOGSPOT.COM

Fidia yakwamisha upanuzi wa kiwanja cha ndege Kigoma



Kiasi cha Sh milioni 473 kinahitajika ili kulipa fidia ya ziada kwa wananchi wanaopaswa kuondoka ili kupisha upanuzi wa uwanja wa ndege wa Kigoma. 

Hatua hiyo ilikuja baada ya wananchi kuweka pingamizi mahakamani wakidai malipo fidia waliyolipwa awali ni madogo.

Akitoa taarifa kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa, Meneja wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege (TAA) mkoani Kigoma, Mohammed Suleiman alisema hatua ya kuongeza fedha hizo za ziada inalenga kumaliza malalamiko ya fidia yanayoukabili mradi huo.

Suleiman alisema katika mpango huo wanatarajia kutoa nyongeza ya Sh 500,000 kwa kila mwananchi anayetakiwa kupisha upanuzi wa uwanja huo, hatua itakayowafanya wananchi waondoe kesi mahakamani na hivyo ujenzi kuanza.

Alisema kiasi cha Sh milioni 650 zilishalipwa kama fidia kwa nyumba, viwanja, mashamba na mazao na kiasi cha Sh milioni 645 zililipwa kama fidia kwa makaburi 2,786. 

Meneja huyo wa TAA alisema kuwa utekelezaji wa mradi wa upanuzi wa njia ya kurukia ndege utawezesha njia hiyo kufikia mita 3,100 na hivyo kuwezesha ndege kubwa ikiwemo Boing 737 kutua na kwamba kwa sasa awamu ya kwanza ya mradi huo imewezesha njia hiyo kufikia mita 1800.

Alisema mradi wa jengo la kisasa la abiria na mnara wa kuongozea ndege unatarajiwa kuanza mwezi Julai mwaka huu na kwamba michakato ya utekelezaji wa mradi huo inaendelea kwa hatua mbalimbali.

Akizungumzia taarifa hiyo, Mbunge wa Jimbo la Kigoma Mjini, Zitto Kabwe, alieleza kusikitishwa kwake na tabia ya baadhi ya wananchi wa Manispaa ya Kigoma Ujiji kupenda kuzuia miradi ya maendeleo mahakamani kwa kulalamikia fidia.
 
 
chanzo>mpekuzi
Share on Google Plus

News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook , Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.

0 comments:

Post a Comment