Hatimaye Shirika la Posta Nchini
kufikisha huduma za Posta Mlangoni, ili kuendana na kasi ya awamu ya
tano katika kuchangia ongezeko la uchumi wa kati nchini ifikapo 2025.
Akizungumza jijini Dar es Salaam Kaimu
Posta Masta Mkuu wa Shirika la Posta nchini Fortunatus Kapinga, amesema
kuwa huduma hii itawawezeha wateja wenye anuani sahihi za makazi
kufikishiwa barua, vifurushi na vipeto kwa urahisi zaidi tofauti na
zamani ambapo ilimlazimu mteja afike katika ofisi za Posta na ilichangia
upotevu wa vitu hivyo.
Akizungumzia hatua zilizofikiwa na
Serikali kuhusu huduma hiyo Kaimu Posta Masta Mkuu huyo ameeleza kuwa
mpaka sasa wamezifikia kata 32 kwa mkoa wa Dar es Saalam, Arusha 8 huku
Zanzibar zikifikiwa kata 6 mbili za Unguja na nne za Pemba.
Wakati huduma hiyo ikitarajiwa
kuzinduliwa siku ya Jumanne Kaimu Mkuu Kapinga ameitaja baadhi ya mikoa
ambayo itafuatia kwa kuwekewa huduma hii ni Mwanza, Tanga, Morogoro,
Kagera, Mara, Mtwara, Lindi,Shinyanga, Pwani, Manyara, Simiyu na Geita,
pamoja na Tanzania Visiwani Unguja na Pemba kwa awamu ya pili, huku
awamu ya Tatu ikijumuisha mikoa ya Songwe, Kigoma, Singida, Rukwa,
Ruvuma, Katavi na Njombe kwa mwaka 2017 – 2018
News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook, Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.
RELATED POSTS
Huduma za Posta kuwafikia wateja mlangoni
Reviewed by Newspointtz
on
14:39:00
Rating: 5
0 comments:
Post a Comment