Madiwani wa chama cha demokrasia na maendeleo Chadema wilayani kyela
wamekubaliana kufanya usafi wa mazingira kila mwisho wa wiki ikiwa ni
kuunga mkono juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa tanzania John
pombe magufuli kufanya usafi kila mwisho wa mwezi.
Mratibu wa zoezi
hilo ambaye ni diwani wa kata ya mbugani Claud Fungo amesema wameamua
kuunga mkono kauli ya hapa kazi tu kwa vitendo tofauti na baadhi ya
viongozi wa serikali kushindwa kufanya kazi na kubaki kuwasimamia wananchi .
Kwaupande wake diwani wa kata ya mikoroshoni Bruno sanga na madiwani
kutoka katika kata za nkuyu na itunge wamesema kujikitokeza kwao
kufanya usafi wa mazingira kutawahamasisha wananchi kufanya shughuli za
maendeleo pamoja na kutokomeza ugonjwa wa kipindupindu ambao umekuwa
ukiibuka mara kwa mara wilayani hapa.
Naye mwenyekiti wa kitongoji cha
butiama Anton Mapunda ameamua kuungana na zoezi hilo linaloendeshwa na
madiwani wa chadema kwa kuwa yeye ni muumini wa maendeleo na kutoa wito
kwa viongozi wengine kujitoa ili kufanya waliyowaahidi wananchi.
Zoezi la
kufanya usafi kila mwisho wa wiki ambalo litafanywa na madiwani wa
chadema litafanyika kwa kila kata iliyopo wilayani hapa ikiwa ni pamoja
na kufanya usafi mashuleni,katika vituo vya afya na zahanati ili
kuhakikisha kyela inakuwa safi na kutokomeza ugonjwa wa kipindupindu
kinachosababishwa na uchafu.
0 comments:
Post a Comment