Tukio hilo limetokea wakati Al Ahly ilikuwa ikifanya mazoezi ambapo mara baada ya kukuta geti limefungwa mashabiki hao wasiopungua 45 waliamua kuruka ukuta na kumkuta mwandishi wa Azam Media Gedion Mkude na kuanza kumshambulia wakimzuia kuwachukua kwa kamera yake.
Baada ya tukio hilo Gedion alitoa taarifa kwa Meneja wa Uwanja ambaye naye alimpigia simu mkuu wa kituo cha Chang’ombe ambaye alifika na kuwachukua mashabiki hao ambao hata walipokamatwa hawakuonekana kujali chochote
Mpaka Shaffihdauda inaondoka katika kituo cha Chang’ombe baadhi ya mashabiki hao walikuwa wakiendelea kutoa maelezo juu ya tukio hilo.
0 comments:
Post a Comment