NEWSPOINTTZ.BLOGSPOT.COM

NEMC Yakipiga Faini ya Milioni 20 Kiwanda cha Karatasi Mufindi (MPM)


Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Kanda ya Nyanda za Juu Kusini limekitoza faini ya shilingi milioni 20 Kiwanda cha Karatasi Mufindi (MPM) kilichopo kijiji cha Mgololo kata ya Makungu katika Halmashauri ya wilaya ya Mufindi mkoani Iringa baada ya kushindwa kufanya maboresho katika mfumo wake wa kuchuja maji taka kabla ya kuingia kwenye mto licha ya kuagizwa kufanya hivyo mara kadhaa.

Bw. Godlove Mwamsojo ambaye ni Mratibu wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Kanda ya Nyanda za Juu Kusini amesema adhabu hiyo ambayo ni kwa mujibu wa sheria ya mazingira ya 2014 vifungu vya 186 na 198 inapaswa kutekelezwa katika kipindi cha siku 14.

Amesema kiwanda hicho pekee cha uzalishaji wa karatasi nchini kimeshindwa kudhibiti maji taka yanatoka kiwandani hapo na kutiririshwa katika mto Kigogo hali ambayo amesema inayaweka rehani maisha ya watu na viumbe wengine wanaotumia maji ya mto huo.

Kwa upande wake Naibu Waziri Nchi Ofisi ya Makamu wa Raisi Muungano na Mazingira, Bw. Luhaga Mpina amewataka wenye viwanda nchini kukidhi mahitaji ya sheria mbalimbali ikiwemo ya mazingira sambamba na kuikumbusha NEMC kufanya kazi usiku na mchana bila kuchoka.
Share on Google Plus

News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook , Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.

0 comments:

Post a Comment