NEWSPOINTTZ.BLOGSPOT.COM

RAAWU Kujitoa zaidi kutetea wanachama wake


Mwenyekiti wa kamati ya wanawake kanda ya kati(RAAWU) Bi. Gaudincie Leo Donati,Jana katika kikao cha tathimini ya chama hicho kilicho fanyika kwenye viwanja vya bwalo la( JKT) mjini Morogoro aliwataka wajumbe wa kikao kuthamini jitihada zinazo fanywa na chama katika kutetea wanachama wake.

"Ukiwa kiongozi unatakiwa utambue majukumu yako, na kazi yetu kubwa ni kuwatetea wanachama kwetu" Alisema Bi.Gaudiencia Leo Donati.

Katika kikao hicho cha tathmini mjumbe wa RAAWU tawi la chuo kikuu cha kilimo(SUA) Bi. Hidaya Ahmadi kwa niaba ya wajumbe wenzake walimuomba mwenyekiti wa kamati ya wanawake 
Bi. Gaudiencia Leo Donati ambaye anamaliza muda wake, aweze kuwakubalia wajumbe aendelee kugombea nafasi hiyo na wote kwa pamoja wamuunge mkono.

"Mwenyekiti pamoja umesema hiki ndio kikao chako cha mwisho ukiwa kama mwenyekiti wa kamati ya wanawake kanda, sisi hapa kwa umoja wetu yupo tayari kukuchukulia fomu na kujaza uweze kuendelea kutuongoza" alisisitiza Bi.Hidaya Ahmadi.

Naye katibu wa RAAWU mkoa wa Morogoro, ndugu Baraka Issa aliwataka wajumbe wajiweke tayari kwa maandalizi ya siku wa wafanyakazi itakayo fanyika siku tarehe 1 mwezi wa 5 ambayo kimkoa itafanyika Morogoro na kitaifa itafanyika Dodoma.

" mjiweke tayari kwa maandalizi ya ya mei mosi, na kwa tathimini hii iwe mwongozi wetu katika shughuli zinazofuata" Aliongezea ndugu Baraka Issa.
 
Kikao hicho kilifanyika kufanya tathimini ya kuangalia namna chama kilivyo adhimisha siku ya wanawake Duniani inayo adhimishwa kula ifikapo 8/3

Share on Google Plus

News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook , Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.

0 comments:

Post a Comment