Staa wa filamu Bongo, Shamsa Ford.
STAA wa filamu Bongo, Shamsa Ford juzikati amemsweka lupango mzazi
mwenziye Dick Matoke, katika Kituo cha Polisi cha Oysterbay kwa kile
kinachodaiwa kuwa mzazi mwenzake huyo kuwa na tabia ya kumtukana mara
kwa mara akishirikiana na mpenzi wake wa sasa ambaye jina lake
halikuweza kupatikana mara moja.
Kwa mujibu wa chanzo makini, Dick
na mwanamke wake wa sasa wamekuwa wakimtumia meseji za matusi Shamsa
kitendo ambacho mwigizaji huyo alikuwa akikivumilia lakini katikati ya
wiki hii, uvumilivu ukamshinda, akaamua kwenda kumshtaki.
“Yaani
hakuna kitu ambacho Shamsa alikuwa hakipendi kama kutumiwa meseji na
mzazi mwenzake huyo na mwanamke wake zikimtusi kwa maana alivumilia
mpaka akachoka, akaona bora aende polisi kumshtaki,” kilisema chanzo.
Shamsa Ford enzi akiwa na mzazi mwenziye Dick Matoke.
Shamsa Ford enzi akiwa na mzazi mwenziye Dick Matoke.
Chanzo hicho kilizidi kueleza kuwa, baada ya kwenda polisi na kufungua
mashtaka yaliyosomeka; OB/RB/6522/2016, usiku wa Aprili 6, mwaka huu,
polisi walikwenda nyumbani kwa Dick maeneo ya Mikocheni jijini Dar
ambapo walifanikiwa kumkuta, wakampeleka kituoni Oysterbay.
“Polisi
wanaendelea kumtafuta na mpenzi wa Dick aliyekuwa akishirikiana naye
kumtukana Shamsa ili naye waweze kumhoji kisha hatua nyingine za
kisheria zichukue mkondo wake,” kilisema chanzo hicho.
Alipotafutwa
Shamsa kuhusiana na sakata hilo, alikiri kutokea lakini akaomba muda ili
alizungumze vizuri kwa kile alichosema yuko bize na shughuli zake za
filamu.
“Mh! Umeipata hiyo na wewe? Nani aliyekuambia? Any way ni
kweli imetokea lakini nitakuelezea vizuri nikitulia, niko bize kidogo
na kazi,” alisema Shamsa.
0 comments:
Post a Comment