Hatimaye
tatizo la umeme lililotokea katika Hospitali ya Taifa Muhimbili mnamo
Machi 28 mwaka huu lapatiwa ufumbuzi baada ya umeme kurejea katika hali
ya kawaida.
Katika
taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Umma wa
Hospitali ya Taifa Muhimbili Aminieli Aligaesha jana ofisini kwake
Jijini Dar es salaam , amesema kukosekana kwa umeme hospitalini hapo
kumetokana na waya mkubwa wa kusambaza umeme kupata hitilafu.
“Tayari
waya umeshabadilishwa na kuwekwa waya mpya, mpaka sasa kazi imekamilika
na huduma zinaendelea kama kawaida”alisema Aligaesha.
Aidha
, Aligaesha alikanusha juu ya taarifa ya kifo cha mama mjamzito kuwa
alikosa huduma akiwa katika chumba cha upasuaji kwasababu ya tatizo la
kukatika kwa umeme .
“Napenda
kutaarifu umma kwamba taarifa hii siyo ya kweli bali ni upotoshaji
kwani kifo cha mama huyu kilitokana na sababu za kitaalamu”alisema
Aligaesha.
Imeandaliwa na Jacquiline Mrisho
0 comments:
Post a Comment