Mshambuliaji wa Yanga Donald Ngoma
amewaomba mashabiki wa Yanga kujitokeza kwa wingi Uwanja wa Taifa, Dar
es Salaam kesho wakati Yanga itakapokuwa inapata ushindi dhidi ya Al
Ahly mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika.
Mshambuliaji huyo aliyetua Yanga msimu
huu akitokea timu ya Platinum ya Zimbabwe, alisema lengo lake ni kuona
Yanga inapata ushindi mnono kesho.
Alisema anafurahi mashabiki wa Yanga
wamempokea vizuri na namna ya kuwalipa ni kuwafanyia kazi itakayowapa
furaha na mojawapo ni kuifunga Al Ahly kabla hawajakwenda kurudiana
nchini Misri.
Pia amesema ndoto yake nyingine ni
kuipa Yanga taji la ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara, jambo ambalo
anaamini linawezekana. Ngoma ambaye ameshaifungia Yanga mabao 15 mpaka
sasa, alisema hata mabao yake anayofunga sasa hayatakuwa na maana kama
Yanga haitashinda taji la Ligi Kuu ya Soka ya Tanzania Bara msimu huu.
“Hata haya mashindano ya kimataifa
tunayoshiriki sasa ni kwa sababu wenzetu walishinda ubingwa msimu
uliopita, na mimi lengo langu ni kushinda taji kwenye msimu wangu wa
kwanza ili tuendelee kushiriki mashindano ya kimataifa msimu
ujao,”alisema Ngoma.
News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook, Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.
RELATED POSTS
Tutaifunga Al Ahly na Ubingwa VPL Wetu-NGOMA:
Reviewed by Newspointtz
on
11:55:00
Rating: 5
0 comments:
Post a Comment