Wananchi
wa wilaya ya Kyela wametakiwa kuachana na mila potofu na kupelekea
kufanya mauaji ya watu kwa kuhusisha ugonjwa wa kipindupindu ni ugonjwa
unaoletwa kwa imani ya kishirikina
Hayo
yamesemwa leo na waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na
Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu, wakati alipofanya ziara katika wilaya hii na
kuongea na watendaji wa halmashauri.
Mhe.Ummy alisema ameshangazwa na baadhi ya wananchi katika kijiji cha
Unyakyusa kujichukulia sheria mkononi na kuwauwa wanawake watatu kwa
madai ndio wanaoneza ugonjwa huo.
Naye
mkuu wa wilaya ya Kyela, Dkt. Thea Ntara alisema kamati yake ya ulinzi
na usalama imeshawakamata watuhumiwa wawili wa tukio hilo na kuwafikisha
mahakamani ingawa bado mtuhumiwa mmoja aliyekimbilia nchi jirani ya
Malawi anatafutwa.
Matukio hayo yametokea mwezi Februari na Machi mwaka huu.
Wilaya ya Kyela ilipokea mgonjwa wa kipindupindu Novemba, 2015 na hadi kufikia Machi, 2016 jumla ya wagonjwa 405 waliugua ambapo vifo vilikua 8. Kwa sasa wilaya hii haina mgonjwa wa kipindupindu.
Pia Waziri Ummy Mwalimu ameahidi kuwapelekea dawa za kutibu maji (water guard) wananchi wa Kyela
Hali
ya kipindupindu nchini imekua ni tatizo kubwa nchini, takribani mikoa
yote Tanzania bara imekubwa na ugonjwa huu tangu ulipotiwe mwezi Agosti mwaka jana, isipokuwa kwa mkoa wa Ruvuma na Njombe ambapo hawajaripoti mgonjwa wowote hadi sasa.
Ripoti
ya wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto ya Machi,
4 mwaka huu inaonesha jumla ya wagonjwa 20,294 wametolewa taarifa na
kati ya hao 320 wamepoteza maisha.
Kwa kipindi cha robo ya kwanza ya mwaka, mwenendo wa kipindupindu unaashiria idadi ya wagonjwa nchini kuongezeka.
Na Catherine Sungura, Kyela
Waziri
Ummy Mwalimu akiongea na watendaji wa wilaya ya Kyela,kushoto ni makamu
mwenyekiti wa wilaya, Stephen Mwangalaba na kulia ni Mkuu wa Wilaya
hiyo, Dkt. Thea Ntara.
Mkuu wa Wilaya hiyo, Dkt. Thea Ntara akizungumza na watumishi wa wilaya ya Kyela.
Baadhi
ya wauguzi wa hospitali ya wilaya wakimsubiri kumpokea waziri wa Afya,
Mh.Ummy Mwalimu amewakumbusha watoa huduma hao kuwahudumia wananchi kwa
kufuata weledi wa taaluma zao.
Waziri
wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu
akisalimiana na watoa huduma wa hospitali ya wilaya ya Kyela.
Waziri
Ummy Mwalimu akipata maelezo kwenye dirisha la wanaotumia kadi ya mfuko
wa wa jamii( CHF) toka kwa mhudumu (hayupo pichani) wa hospitali ya
wilaya ya Kyela.
0 comments:
Post a Comment