Katika
kukabiliana na upungufu wa uzalishaji wa umeme wa kutosha serikali
imefanya mapitio ya ripoti ya kuendeleza nishati ya joto ardhi kwa lengo
la kuongeza uzalishaji mwingine wa umeme ambao utasaidia kwa
Watanzania kupata dira ya maendeleo na kuongeza maendeleo ya uchumi wa
Taifa .
Akizungumza na Waandishi wa Habari
jijini Dar es Salaam kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini, Prof.
Sospeter Muhongo, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini Dk.
Mhandisi Juliana Pallangyo amesema kuanzisha kwa umeme wa jotoardhi
unaotokana na mwamba wenye joto unaochemsha maji yaliyoingia ardhini
ambapo utasaidia kupunguza kwa kiasi kikubwa uhaba wa umeme hapa nchini
.
Aidha maeneo yaliyolengwa ni Manyara,
Ngozi Ngorongoro, Kisaki Majimoto Mara na mengineyo ambapo mvuke wake
ni msafi na hauna madhara yeyote ambayo huweza kutumika kwa matumizi
mbalimbali ya nyumbani , viwandani kilimo na dawa .
Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa
Kampuni ya kuendeleza Jotoardhi Tanzania (TGDC) Mhandisi Boniface Njombe
amesema kuwa ilianzishwa Desemba 2013 kwa madhumuni ya kusimamia na
kuongeza maendeleo ya ya jotoardhi nchini ambapo kuzalisha megawaiti 200
ifikapo mwaka 2020 na mega waiti 500 ifikapo mwaka 2025 na 2033
itazalisha megaweti 800 .
News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook, Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.
RELATED POSTS
Serikali yaja na mkakati mpya kuongeza umeme nnchini
Reviewed by Newspointtz
on
06:57:00
Rating: 5
0 comments:
Post a Comment