Mamlaka
ya Mapato Tanzania (TRA) imekutana na wafanyabiashara na wawekezaji
kutoka China ambao wanatekeleza miradi mbalimbali hapa nchini lengo
likiwa ni kupeana elimu juu ya utekelezaji wa kipengele cha zuio kwenye
kodi ya mapato kwa makandarasi walio na miradi ambacho kinamtaka kulipa
zuio hilo kabla ya kulipa kodi mwisho wa mwaka.
Akizungumza wakati wa ufunguzi wa semina
ya 14 kwa wafanyabishara hao Meneja Elimu kwa Mlipakodi (TRA) Diana
Masalla amesema kumekuwa na mkanganyiko namna ya kutenganisha kipengele
cha zuio na kodi ya mapato ambacho kinamtaka mkandarasi kutenga
malighafi ambayo yanakatwa zuio asilimia 2 na utaalamu asilimia 5.
Masalla amesema kipengele hiki si kigeni
kipo miaka mingi bali kinashindwa kueleweka miongoni mwa wahusika na
kinazihusu taasisi za serikali zinapokea ruzuku hivyo ni vema kila mmoja
akaelewa kabla ya kutekeleza miradi mbalimbali hapa nchini.
News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook, Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.
RELATED POSTS
TRA YAKUTANA NA WAFANYABIASHARA NA WAWEKEZAJI WA CHINA
Reviewed by Newspointtz
on
07:15:00
Rating: 5
0 comments:
Post a Comment