NEWSPOINTTZ.BLOGSPOT.COM

Basata wameshindwa kunipa majibu ya msingi – Roma


Roma
Msanii wa Hip Hop Bongo, Roma amesema kuwa Baraza la Sanaa la Taifa, Basata limeshindwa kumpatia majibu ya msingi juu ya sababu ya kufungiwa kwa nyimbo yake ya ‘Viva Roma Viva’.

Msanii huyo amekiambia kipindi cha ‘Hatua Tatu’ cha Times FM kuwa Basata wameshindwa kumpa sababu za msingi juu ya kufungia wimbo wake.

“Siwasemei wengine lakini mimi nilijaribu kuwauliza Basata kwanini wamefungia wimbo wangu lakini sikupewa majibu ya msingi na yenye kueleweka,” alisema Roma.

Basata waliufungia wimbo wa Roma ‘Viva Roma Viva’ mwezi October mwaka jana kwa madai kuwa wimbo huo umekiuka maadili kutokana na kuchochea ugomvi.
Share on Google Plus

News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook , Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.

0 comments:

Post a Comment