NEWSPOINTTZ.BLOGSPOT.COM

Bodi ya Utalii yasisitiza Mlima Kilimanjaro upo Tanzania

Bodi ya Utalii nchini imetoa taarifa kufafanua kuhusu mlima Kilimanjaro baada ya shirika moja la habari la Marekani kudaiwa kuchapisha taarifa iliyoonekana kuashiria mlima huo unapatikana Kenya.

Taarifa hiyo imekuja baada ya kutokea kwa kifo cha dereva wa kimataifa wa mbio za magari Guguleth Zulu, aliyefariki dunia wakati akipanda Mlima Kilimanjaro.

Kwa mujibu wa taarifa ya bodi ya utalii kwa vyombo vya habari imekanusha taarifa iliyochapishwa na mwandishi wa shirika la AP kwamba milma huo upo Kenya.

‘’Tungependa kusahihisha habari za kupotosha kwamba mlima Kilimanjaro unapatikana Tanzania na si Kenya,”

Aidha Bodi ya Utalii Tanzania imeandika barua kwa chombo cha habari kilichofanya makosa hayo na kutaka wafanye marekebisho.

Miezi michache iliyopita mtoto wa aliyekuwa Waziri Mkuu wa Kenya Raila Odinga, Rose Mary Odinga akihutubia vijana nchini Marekani aliwaambia Olduvai Gorge ipo Kenya na baadaye alikanusha taarifa hiyo.
Share on Google Plus

News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook , Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.

0 comments:

Post a Comment