NEWSPOINTTZ.BLOGSPOT.COM

Kiwanda Cha Nguo Cha 21st Century Chateketea Kwa Moto

BAADHI ya mitambo, nguo na malighafi katika Kiwanda cha Nguo cha 21st Century kilichopo Kihonda, Morogoro vimeteketea kwa moto na kusababisha hasara.

Akizungumzia moto huo Clement Munisi, meneja uzalishaji wa kiwanda hicho amesema kuwa, moto huo ulianza saa 12:00 asubuhi leo katika  mashine moja ya kuzalishia  nguo kwa ulianza kwa kutoa cheche.

Amesema, wafanyakazi walijaribu kuuzima kwa kutumia kifaa maalumu cha kuzima moto (Fire extinguisher ) bila mafanikio yoyote.

Munisi amesema kuwa, moto huo uliunguza baadhi ya mitambo na malighafi zilizokuwa katika chumba kimoja ndani ya kiwanda hicho na kusababisha hasara kubwa.

Amesema kuwa, moto huo uliendelea kuenea katika vyumba vingine ndani ya kiwanda hicho jambo ambalo lililosababisha baadhi ya nguo zilizokuwa zikiendelea kutengenezwa kuungua. Hata hivyo, hajaeleza dhamani halisi ya vitu vilivyoteketea kwa moto.

Ramadhani  Pilipili, Kamanda wa Kikosi cha Zimamoto  Mkoa wa Morogoro amesema kuwa, licha ya kuwahi kufika mapema katika eneo la tukio na juhudi za kuuzima moto, bado miundombinu ya kiwanda hicho imekuwa  kikwazo.

“Miundombinu ya kiwanda ni tatizo kutokana na kukosekana eneo sahihi la kupitishi mipira ya maji na hivyo kulazimika kutumia muda mwingi kwa kuvunja ukuta ili kufanikisha zoezi la uzimaji,” amesema.
Share on Google Plus

News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook , Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.

0 comments:

Post a Comment