NEWSPOINTTZ.BLOGSPOT.COM

Mourinho katoa Top 3 ya wachezaji wake wa muda wote anao wakubali

071916-SOC-real-madrid-cristiano-ronaldo-jose-mourinho.vadapt.664.high_.86
Kocha wa Man United Jose Mourinho ametoa list ya wachezaji wake watatu wa muda wote na kumuacha Ronaldo baada ya kutoa list hiyo imekuwa gumzo katika mitandao ya kijamii, Mourinho katika mahojiano na Daily Express ametaja majina ya wachezaji wake watatu wa muda wote.
071916-SOC-real-madrid-cristiano-ronaldo-jose-mourinho.vadapt.664.high_.86
Mourinho amewataja Messi, Pele na Diego Maradona kama ndio wachezaji bora wa muda wote na ameonekana amempotezea mreno mwenzake Cristiano Ronaldo ambaye watu wengi walizani kuwa atakuwemo katika list hiyo ya Mourinho ukilinganisha uwezo wake na utaifa wao “Kwangu mimi binafsi TOP 3 ya wachezaji bora wa muda wote katika historia ni Messi, Pele na Maradona”
Ronaldo amewahi kufundishwa na Mourinho kwa misimu mitatu katika klabu ya Real Madrid na mwaka 2012 alifanikiwa kushinda tuzo ya Ballon d’Or akiwa chini ya Mourinho, kauli hiyo ya Mourinho inaonyesha kuwa na tofauti na Ronaldo lakini wengi hawakutarajia kuona Ronaldo akikosekana katika list hiyo.
Share on Google Plus

News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook , Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.

0 comments:

Post a Comment