NEWSPOINTTZ.BLOGSPOT.COM

Mtoto wangu wa kike ataitwa Karma – Wema

Malkia wa filamu Wema Sepetu bado hajakata tamaa kuhusu kupata mtoto licha ya kukatishwa tamaa na baadhi ya watu katika mitandao ya kijamii kutokana na uzazi wake kuwa mgumu.
wema
Muigizaji huyo ambaye alianzisha mfumo wa APP na SMS ambao unatoa taarifa zake mbalimbali kwa mashabiki juu ya maisha yake, tayari umeanza kutoa taarifa mbalimbali kuhusu maisha yake.
Kupitia mfumo huo, Wema amesema angependa mwanae wakiume ampatie jina la Karma.
“Mtoto wangu wa kiume ataitwa Karma,” alisema Wema. “Bado sijafikiria jina nitakalo mpa mtoto wangu wa kiume japo namtaka sana mtoto wa kwanza awe wa kiume, Mungu anajua,” alisema Wema.
Pia kupitia system hiyo, Wema amewashukuru mastaa wenzake wa filamu ambao walimsupport katika show yake ya ‘The Black Tie’.
Share on Google Plus

News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook , Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.

0 comments:

Post a Comment