NEWSPOINTTZ.BLOGSPOT.COM

WACHEZAJI WALIOFANIKIWA KUFUNGA MAGOLI MATATU KWA DAKIKA CHACHE

Katika michezo kuna vitu vingi haswa katika magoli kuna kitu kinaitwa ‘hat-tricks’ yaani mchezaji kufunga magoli matatu kwa mchezo mmoja na zawadi yake kuondoka na mpira uliokuwa unatumika katika mchezo huo, ili kutoa thamani kwa mfungaji.Davida Villa

Sheria hii ni nzuri mno haswa kutoa hadhi kwa kufunga magoli matatu, maana sio rahisi kufunga magoli 3 kwa mchezo mmoja, hivyo waliotunga sheria hii wanatakiwa wapongezwe kwa kuangalia thamani katika michezo. Zifuatazo ni ‘hat-tricks’ zilizofungwa kwa dakia chache. Cristiano Ronaldo na Lionel Messi peke yao ndio wanaweza kufunga ‘hat-tricks’ kwa furaha tu ila mchezaji wakawaida kazi ngumu.

1. ANDY CARROL

Mchezaji wa zamani wa vilabu vya Newcastle United, Liverpool na sasa Westham United aliifunga Arsenal mwaka 2016 kwa kutumia dakika 7 ambapo mchezo huo umeisha kwa Arsenal kuambulia sare ya 3-3.ANDY CARROL

2. Matt Mousillou

Mshambuliaji wa Lille ya Ufaransa yeye amefunga hat-tricks kwa kutumia dakika 4 katika ushindi wa magoli 8-0 mwaka 2005.

3. Davida Villa

Huyu mchezaji wa zamani wa Barcelona kwa sasa anacheza MSL Marekani, ameweka rekodi yake mwenyewe hadi leo hii hakuna aliyoivunja  amefunga magoli 3 kwa  dakika 4   mwaka 2005-2006 wakati huo anacheza Valencia.Davida Villa

4. Robert Lewandowski 

Amefunga magoli 5 kwa dakika 8 na hakuna aliye ivunja rekodi hiyo kwa ligi ya Bundasliga mwaka 2015, pia amefunga magoli 3 kwa dakika 3 mwaka huo huo na mchezo huo huo kipindi cha pili.Robert Lewandowski

5. Sadio Mane

Kwa sasa ni mshambuliaji wa Liverpool alifunga magoli 3 msimu wa  2015-2016 akiwa Sauthampton rekodi yake hakuna aliyeivunja kwani alifunga magoli 3 ndani ya dakika 3 yaani 13,14,15 dhidi ya Aston Villa.Sadio Mane

Share on Google Plus

News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook , Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.

0 comments:

Post a Comment