.
Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) limeufungia rasmi wimbo wa ‘pale
kati patamu’ ulioimbwa na msanii Nay wa Mitego kutokana na ukiukwaji
mkubwa wa maadili
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Katibu
Mtendaji wa BASATA, Godfrey Mngereza ameeleza kuwa msanii huyo amekuwa
na tabia na mienendo yenye kuchafua sekta ya sanaa yeye binafsi kupitia
kutoa kazi chafu na kufanya maonyesho yenye kukiuka maadili.
“Kazi zake zikikiuka maadili na kudhalilisha utu wa mwanamke sambamba
na kutoa lugha za matusi na za kudhalilisha watu wa kada mbalimbali.”
alisema Mngereza.
Aliongeza, “Ikumbukwe kwamba BASATA limeshamuita na kumuonya msanii
huyu mara kadhaa kutokana na tabia yake ya kutoa kazi zisizokuwa na
maadili na aliahidi kubadilika na kuachana na tabia hiyo.
Kwa hiyo
kuendelea kwake kufanya matukio haya kwa makusudi ni uthibitisho kwamba
hajabadilika na kwa maana hiyo ameendelea kuidhalilisha sanaa na wasanii
wa kitanzania wenye kujitambua na kuiheshimu kazi ya sanaa kama kazi
nyingine.
Kwa sasa Msanii huyu ametoa wimbo mwingine wa ambao uko
mitandaoni ukipambwa na picha chafu zinazoonesha mwanamke akiwa mtupu
yaani uchi wa mnyama.”
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)
0 comments:
Post a Comment