WAZIRI
Kiongozi mstaafu Zanzibar, Shamsi Vuai Nahodha, amesema Chama Cha
Mapinduzi (CCM) Zanzibar kitakabiliwa na ushindani mkubwa katika
uchaguzi mkuu wa mwaka 2020 kulikoni ule wa mwaka jana.
Nahodha alitoa kauli hiyo jana
alipokuwa akizungumza na watendaji wa CCM Jimbo la Amani katika Tawi la
CCM kwa Wazee Sebleni, akiwa katika ziara ya kukutana na watendaji wa
majimbo akiwa mlezi wa CCM Mkoa wa Mjini Magharibi.
Shamsi alisema uchaguzi ambao matokeo
yake yalifutwa ulikuwa na ushindani mkubwa kati ya CCM na CUF na
kuwataka viongozi na watendaji kufanya matayarisho mapema ya uchaguzi wa
mwaka 2020.
Alisema CUF walijiandaa zaidi na
kufikia kufanya vitendo vya udaganyifu na kusababisha uchaguzi
kuvurugika na kufutwa matokeo ya uchaguzi huo na Mwenyekiti wa Tume ya
Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC), Jecha Salim Jecha.
“CUF watajiandaa zadi kuliko kipindi
kilichopita. Kama walifanya ghiriba mara tatu watafanya mara 10 zaidi,
hivyo lazima tuwe na mipango na mikakati katika kuelekea uchaguzi mkuu,”
alisema.
News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook, Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.
Nahodha ,maneno yake ni sawa na panga linalokata huku linajijuan linaumia enyewe
ReplyDeletehuo ndio ukweli wenyewe