NEWSPOINTTZ.BLOGSPOT.COM

TRA KUKUSANYA KODI NYUMBA HADI NYUMBA

 

kayombo tra

MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) imetangaza kuanza kutembelea nyumba hadi nyumba kuhakiki gharama za upangishaji ili kukokotoa na kukusanya kodi sahihi ambayo ilikuwa haifiki serikalini. Hivyo, wamewataka wananchi kutunza kumbukumbu za mikataba ya pango ili itakapohitajika na maofisa wa mamlaka hiyo wawapatie.

Akizungumza jijini Dar es Salaam  wakati akielezea kuhusu makusanyo ya kodi kwa mwezi Julai, Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi wa TRA, Richard Kayombo alisema hatua hiyo ni moja ya mikakati ya kuongeza ukusanyaji wa mapato. 

 Alisema kwa Julai, TRA imekusanya Sh trilioni 1.055 sawa na asilimia 95.6 ya lengo la kukusanya Sh trilioni 1.103 iliyopangiwa na serikali kwa mwezi huo.

Alisema ikilinganishwa na kipindi kama hiki kwa mwaka jana, TRA ilikusanya Sh bilioni 914 ikiwa ni ongezeko la asilimia 15.43 ya makusanyo ya mwezi huu huku kwa mwaka wa fedha 2016/2017, TRA imepewa lengo la kukusanya Sh trilioni 15.1 ikilinganishwa na lengo la mwaka jana la Sh trilioni 13.32.

“Natoa wito kwa wapangaji na wapangishaji kujiepusha na aina yoyote ya udanganyifu katika suala zima la kodi halisi ya pango kwa kuwa inaweza kuwasababishia kushtakiwa endapo udanganyifu huo utabainika,” alieleza Kayombo.

Share on Google Plus

News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook , Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.

0 comments:

Post a Comment