Shirikisho
la Soka Africa (Caf), limetangaza kuiondoa Chad katika michuano ijayo
kuwania kufuzu kucheza Afcon na mingine yote iliyo chini yake.
Kama
hiyo haitoshi, Caf imetangaza kuitwanga Chad faini ya dolla 20,000
(zaidi ya Sh milioni 44) kutokana na kitendo chake cha kujiondoa katika
michuano ya ya kuwania kucheza Afcon.
Chad ilitarajiwa kucheza kesho dhidi ya Taifa Stars kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam baada ya kuwa imetwangwa bao 1-0 kwao ND’jamena
0 comments:
Post a Comment