|
Dhaira siku za mwisho za uhai wake |
KIPA wa zamani wa Simba SC, Abbel Dhaira amefariki dunia leo baada ya kusumbuliwa na ugojwa wa saratani ya tumbo kwa muda mrefu.
Kipa huyo wa kimataifa wa Uganda, amefariki akiwa nna umri wa miaka 28 nchini Iceland, ambako alikuwa anachezea klabu ya IBV Vestmannaeyjar.
Mlinda
mlango huyo aliyezaliwa Septemba 9, mwaka 1987, Dhaira amechezea klabu
za AS Vita ya DRC, Express na URA za kwao, Uganda, Simba ya Tanzania na
IBV ya Iceland.
|
Abbel
Dhaira (kulia) akibadilishana mikataba na Mwenyekiti wa Kamati ya
Usajili ya Simba SC, Zacharia Hans Poppe wakati anasajiliwa Msimbazi
mwaka 2013 |
Dhaira amekuwa akilazwa na kuruhusiwa hospitali kwa muda kutokana na saratani ya tumbo ambayo imekatisha maisha yake ya soka.
Dhaira
aliyechezea Simba kwa msimu mmoja wa 2013/2014 kabla ya kurejea Ulaya,
alianza kupatiwa matibabu mapema mwaka huu baada ya klabu yake, IBV
Vestmannaeyjar kuchangisha fedha kwa ajili hiyo, lakini wakati huo hali
yake tayari ilikuwa mbaya sana.
Dhaira,
alianza kuchezea timu ya taifa ya Uganda mwaka 2009 na akacheza Kombe
la CECAFA Challenge mwaka 2012, ambako alikimbizwa hospitali na kulazwa
baada ya kuzimia kufuatia kugongana na mchezaji mwenzake.
Pole kwa
familia yake na Waganda wote. Mungu ampumzishe kwa amani Dhaira. Mbele yake, nyuma yetu. Amin.
0 comments:
Post a Comment