Beki
wa Sunderland, Emannuel Eboue amefungiwa na Shirikisho la Soka Duniani
(FIFA) kujihusisha na soka kwa kipindi cha mwaka mmoja kutokana na
kutokea mzozo wa mkataba kati yake na wakala wake za zamani, Sebastien
Boisseau.
Aidha
katika taarifa imeyotolewa na FIFA imeeleza kuwa mchezaji huyo kabla ya
kurudi katika soka anatakiwa kumlipa wakala wake wa zamani CHF 30,000
ambayo kwa Tanzania sio chini ya Mil. 68.
“Kamati
ya Maadili ya FIFA imempa adhabu Mr. Eboue pamoja na faini ya CHF
30,000 kwa kushindwa kuzingatia sheria za wachezaji kwa kuvunja Kifungu
64 cha Kanuni za maadili ya FIFA,
“Pia
mchezaji anapewa muda wa neema wa siku 120 kukaa na wakili wake wa
zamani, Mr. Boisseau na kumaliza tofauti zao kama itashindikana Mr.
Eboue atapewa adhabu ya kutokujihusisha na shughuli yoyote ya soka kwa
kipindi cha mwaka mmoja,”
Aidha klabu yake ya Sunderland inataraji kumwandikia barua ya kusimamisha mkataba na mchezaji huyo wa zamani wa Arsenal.
0 comments:
Post a Comment