Tanzania inaongoza miongoni mwa nchi 15
za kiafrika katika mradi wa utoaji wa huduma bora za Afya kwa
jamii,Mazingira ya kufanyia kazi na jinsi ya kuzipatia ufumbuzi
changamoto zinazowakabili wagonjwa unaofadhiliwa na shirika la misaada
la kimataifa la Japan (JICA).
Mkufunzi wa kitaifa wa mradi huo
unaojulikana kama 5 s Bi.Salome Saria amesema,tathimini iliyofanywa na
makao makuu ya JICA baada ya miaka kumi ya utekelezaji tanzania
imeonekana kufanya vizuri zaidi kati ya nchi hizo.
Bi Saria amesema hayo katika taarifa
yake kwa maafisa wa JICA Tanzania wanaofuatilia utekelezaji wa mradi huo
katika Hospitali ya rufaa ya KCMC ambao sasa umeanza kutoa huduma
katika vyuo vikuu ya tiba vilivyopo KCMC na maendeo mengine nchini.
Mwenyekiti wa kamati ya mradi huo
Dkt.Mosi Mwasamwaja ameyataja baadhi ya mafanikio ya mradi kuwa ni
pamoja na usalama wa wagonjwa ukiwemo upatikanaji wa dawa, ukuboresha
mazingira ya kufanyia kazi, kupunguza kero za wafanyakazi na kuondoa
mtazamo chanya wa kulaumu uongozi.
Mradi wa mradi huo kutoka ofisi ya JICA
Tanzania Bi Christine Shirima amesema, wameamua kusaidia mradi huo
unaosimamiwa na wizara ya afya ili kuboresha huduma za afya kwa
wafanyakazi wa Tanzania na nchi nyingine za Kiafrika.
News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook, Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.
RELATED POSTS
HUDUMA BORA ZA AFYA ZAIPAISHA TANZANIA KIMATAIFA
Reviewed by Newspointtz
on
09:05:00
Rating: 5
0 comments:
Post a Comment