Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye
Jumamosi hii katika ukumbi wa Golden Jubilee Tower (PSPF Tower) jijini
Dar es salaam amepamba uzinduzi wa video mpya ya wimbo ‘Sizonje’ wa
Mrisho Mpoto.
Uzinduzi huo uliambatana na mdahalo wa
kuwatia moyo wanafunzi waliofeli kidato cha nne ambapo wazungumzaji
mbalimbali kama Waziri Nape Nnauye, Mtangazaji maarufu wa radio ya
Clouds FM Millard Ayo, Mkurugenzi wa vipindi na Uzalishaji wa Clouds FM
Ruge Mutahaba, Mrisho Mpoto pamoja na wanafunzi waliofeli na waliofaulu,
waliweza kuzungumzia dhana ya kufeli shule sio mwisho wa maisha
Akizungumza na wadau waliyojitokeza
katika uzinduzi huo, Mh Nape alisema anafurahishwa na jinsi Mrisho Mpoto
anavyoweza kuitumia sanaa yake kwa ajili ya kuijenga jamii.
“Hii kazi anayofanya Mpoto ndio kazi yangu, kwa hiyo lazima aungwe mkono,”
alisema Nape huku akimwagia sifa msanii huo ambaye kwa sasa yupo kwenye
kinyang’anyiro cha tuzo za KORA kama wasanii bora wa muziki wa asili
Afrika
Pia Nape aliendesha harambee ndogo ya
kuuza DVD mpya za video ya wimbo Sizonje na kufanikiwa kuuza zaidi ya
DVD 7 kwa milioni nane na nusu huku mwenyewe akinunua moja kwa milioni
2. Angalia picha.
News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook, Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.
RELATED POSTS
NAPE AFANYA YAKE UZINDUZI WA VIDEO YA SIZONJE YA MRISHO MPOTO
Reviewed by Newspointtz
on
12:25:00
Rating: 5
0 comments:
Post a Comment