Mbunge wa Jimbo la Mikumi Mkoani
Morogoro Joseph Haule amefanikiwa kupunguza tatizo la maji kwa wakazi wa
jimbo hilo kwa kuchimba Kisima kikubwa kitakachowawezesha wakazi wa
Mikumi kupata maji yaliyo safi na salama.
Mh Haule amesema kuwa amelazimika
kuchimba kisima hicho ili kupunguza tatizo la maji wakati wakiendeleaa
kutathmini namna nzuri zaidi ya kusambaza mabomba na kumaliza kabisa
tatizo la maji katika mji mdogo wa Mikumi.
Jimbo la Mikumi hususan eneo la mji
mdogo wa Mikumi kumekuwa na tatizo la maji kwa takribani miaka kumi sasa
hali inayopelekea wanachi kununua maji lita ishirini kwa shilingi mia
tano huku wengine wakilazimia wakazi wa mji huo kutembea umbali mrefu
kutafuta maji.
News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook, Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.
RELATED POSTS
PROF JAY AZIDI KUTATUA KERO MIKUMI
Reviewed by Newspointtz
on
14:02:00
Rating: 5
0 comments:
Post a Comment