MATAJIRI
wa Ufaransa, Paris Saint-Germain wanaitaka huduma ya mchezaji mwenye
thamani ya Pauni Milioni 45, mshambuliaji wa Liverpool, Daniel
Sturridge.
Msafara
kutoka klabu hiyo ya Paris unatarajiwa kuwasili London kuhudhuria mechi
kati ya England na Uholanzi Uwanja wa Wembley leo.
Sturridge anatarajiwa kucheza sehemu ya mchezo huo baada ya kurejeshwa kikosini. Kocha wa PSG,
Laurent Blanc atakuwa sokoni kusaka mshambuliaji mpya kutokana na
Zlatan Ibrahimovic na Edinson Cavani kuhofiwa kuwa mbioni kuondoka.
Na Sturridge jina lake limo katika orodha ya wachezaji wanaotakiwa PSG, ingawa amebakiza miaka mitatu katika Mkataba wake Merseyside.
0 comments:
Post a Comment