RAIS
wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania dkt
John Pombe Magufuli ametoa zawadi ya pasaka kwa wazee wasiojiweza huku wakisumbuliwa na maradhi ya ugonjwa wa ukoma nakulelewa katika Kambi ya Kolandoto iliyopo manispaa ya Shinyanga.
Zawadi zilizotolewa ni mbuzi wawili,kilo
100 za mchele na mafuta ya kupikia lita 20
vyote vikiwa na thamani ya shilingi 380,000 kwa ajili ya wazee hao 23
baadhi yao wakiwa ni wakisumbuliwa na ugonjwa
wa ukoma na pamoja na watoto 13 wanaishi
katika kambi hiyo.
Akikabidhi zawadi hizo
jana kwa niaba ya Rais,katibu tawala wa
mkoa wa Shinyanga Abdul Dachi alisema rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania
ameona ni vyema kusherehekea sikukuu ya pasaka kwa kuwapatia zawadi wazee hao
ambao baadhi yao ni wagonjwa wa ukoma.
“Kutokana na mheshimiwa
rais kuwa na majukumu mengi amenituma kuwakabidhi zawadi hii ya pasaka
mheshimiwa Rais na familia yake anaungana na wazee wa Kolandoto kusherekea
sikukuu hii ameomba zawadi hii muipokee”alisema katibu tawala Dachi.
Akipokea zawadi hiyo kwa niaba ya wenzake,mwenyekiti wa kambi hiyo mzee Samora
Maganga alimshukuru rais Magufuli kwa kuwakumbuka na kumuomba kuendelea
kusaidia wazee katika jamii kwani wanakumbwa na changamoto mbalimbali ikiwemo
huduma za matibabu katika vituo vya afya.
“Tunamshukuru Rais wetu,ameonesha kujali wazee,tunamtakia
kila heri katika uongozi wake kwani anaonesha kiasi gani yuko pamoja na watu
wananchi wake”,alisema mzee Maganga.
Naye mlezi msaidizi
katika kituo hicho cha wazee Evodia Ndaka alisema kituo hicho kinakabiliwa na
upungufu wa vyumba vya kulala wazee hao kutokana na baadhi ya majengo
kuharibika na kusababisha vyumba vilivyopo kutumiwa na wazee zaidi ya mmoja.
Hata hivyo aliiomba
serikali kuzifanyia ukarabati mkubwa
nyumba za makazi hayo ya wazee kutokana na majengo yake kuchakaa hali
inayowafanya waishi kwa wasiwasi mkubwa na kwamba wamekuwa wakilazimika
kuzihama wakati wa mvua inaponyesha kutokana na kuvuja huku nyingi kati ya hizo
tayari sehemu za kuta zake zimebomoka.
|
0 comments:
Post a Comment