NEWSPOINTTZ.BLOGSPOT.COM

SIMBA YAITUNGUA MBEYA CITY AREJEA KILELENI VPL

 

MABAO ya dakika 75 na 90, yaliyofungwa na Simba leo jioni yameisaidia timu hiyo kupanda kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu Bara na kuzishusha timu za Yanga na Azam, zilizokuwa kileleni.

Simba iliyocheza mchezo huo kwenye Uwanja Taifa jijini Dar es Salaam, ilishuhudia mabao yake yakifungwa na Danny Lyanga na Ibrahim Ajib.

Mchezo huo ulioanza kwa kasi ulishuhudia Mbeya City wakipoteza nafasi ya kufunga bao dakika ya tatu baada ya kupokea pasi kutoka kwa Haruna Moshi ‘Boban’.

Simba ilijibu shambulio hilo dakika ya tano baada ya mshambuliaji wake Ibrahim Ajib, kukosa bao la wazi akishindwa kuunganisha mpira wa Hamis Kiiza ‘Diego’.

Mchezo huo ambao Mbeya City walicheza offside trick, kipindi cha kwanza ulishuhudia Kiiza, akikosa bao la wazi baada ya kupiga mkwaju nje ya 18 na mlinda mlango wa Mbeya City, Hannington Kalysebula kuudaka.

 

Dakik ya 28 Mbeya City, walipata mkwaju wa adhabu ndogo ambao ulienda kupigwa na Haruna Shamte na mpira huo kugonga mwamba wa juu.

Mchezo uliokuwa na mashambulizi ya kushitukiza kwa pande zote, ulishuhudia ukienda mapumziko bila timu kupata bao.

Mchezo huo ukikaribia kwenda mapumziko uliwashuhudia mabeki wa Simba Emiry Nimubona na Juuko Mursheed, wakijichanganya katika kuokoa mpira na Geofrey Mlawa, kushindwa kuifungia bao Mbeya City.

Simba walirudi kipindi cha pili na kufanya mabadiriko ya wachezaji kadhaa ili kuhakikisha wanapata bao, huku mashabiki wa timu hiyo wakilizomea benchi la ufundi kutaka mabadiriko ya wachezaji.

Dakika ya 71, kulitokea mashambulizi ya timu zote kwa Mbeya City nahodha wao Kenny Ally, kupiga mkwaju mkali ambao ulidakwa na Vincent Agban, huku dakika ya 72, Hassan Kessy wa Simba akipanda na mpira na kuchonga krosi iliyoshindwa kutumiwa vyema na Danny Lyanga.

 

Simba, ilijipatia bao hilo pekee baada ya kaazi nzuri iliyofanywa na kiungo mshambuliaji Awadh Juma, aliyeingia uwanjani kipindi cha pili akichukua nafasi ya Kiiza.

Mabadiriko ya kipindi cha pili yaliyofanywa na kocha wa Simba, Jackson Mayanja, ndio yaliyoongeza presha katika lango la Mbeya City na Simba kupata ushindi huo.

Simba: Vincent Angban, Nimubona / Hassan Kessy, Mohamed Hussein ‘Tshabalala’, Mursheed, Novatus Lufunga, Justice Majabvi, Jonas Mkude, Brian Majwega / Danny Lyanga, Mwinyi Kazimoto na Kiiza / Awadh Juma.

 

Mbeya City; Kalyesebula, Hassan Mwasapili, Abubakar Shaban, Tumba Sued, Shamte, Kenny Ally, Raphael Alpha, Moshi / Themi Felix, Geofrey Mlawa, Joseph Mahundi ‘Benteke’ na Ditrim Nchimbi / Ramadhan Chombo ‘Redondo’.

 chanzo>mtembezi

Share on Google Plus

News Point inakusogezea habari kubwa za kila siku kutoka kila kona ya dunia. Ungana nasi kupitia Facebook , Twitter na Instagaram ili uwe wa kwanza kupata habari.

0 comments:

Post a Comment